Je, unahitaji msaada wa matibabu haraka?

Urgent care hupatikana sasa.

Urgent care ni huduma kwa masuala ya kiafya ambayo hayahatarishi maisha lakini yanahitaji uangalifu wa kimatibabu haraka.

Urgent care ni ya bure kwa watu ambao wana kadi za Medicare na watafutaji hifadhi wanaokaa kwenye jamii.

Ili kupata urgent care (huduma ya haraka), piga simu kwa healthdirect bila malipo kwa 1800 022 222, saa 24 kwa siku, siku 7 kwa wiki.

Ili kupata usaidizi wa lugha, pigia simu kwanza kwa TIS Taifa kwa 131 450 na uliza kwa healthdirect.

Healthdirect ni huduma inayofadhiliwa na serikali ambayo hutoa taarifa za afya na ushauri kupitia tovuti, app na simu ya usaidizi.

Muuguzi atajibu simu yako, atakuuliza maswali na kisha kukuunganisha na huduma inayofaa katika mahali pazuri kushughulikia mahitaji yako ya kiafya.

Muuguzi wa healthdirect anaweza:

  • Kukuunganisha na mtaalamu kwa njia ya simu au kwa video.
  • Kukuweka kwa uteuzi katika huduma ya urgent care ya mtaa.
  • Kukuunganisha na huduma nyingine za afya zinazofaa, zinazopatikana karibu nawe , ikiwa ni pamoja na GP au daktari yako wa kawaida.
  • Kupigia simu ambulensi kwa ajili yako au kukuelekeza kwa idara ya dharura ya karibu kama hali yako ni ya dharura.

Je, unahitaji usaidizi wa ziada?

Ikiwa ukihitaji usaidizi wa kusikia au kusema, tembelea tovuti ya National Relay Service kwa Access Hub ili kuchagua mbinu wa kutuma ujumbe kwa zamu ambao unafaa kwako na kisha uliza kwa healthdirect.

Ikiwa una mahitaji mengine ya usaidizi, umwambie muuguzi anayejibu simu yako kwa healthdirect.

Katika hali ya dharura, kila wakati pigia simu kwa Sifuri Mara Tatu (000)

Iwapo suala lako la kiafya linahatarisha maisha, kila wakati pigia simu kwa Sifuri Mara Tatu (000).

Mifano ya dharura yenye kuhatarisha maisha inajumuisha:

  • kuanguka ghafla
  • shinikizo au maumivu ya kifua yanayodumu zaidi ya dakika 10
  • matatizo ya kupumua
  • kutokwa na damu isiyoweza kudhibitiwa
  • matatizo makubwa ya afya ya kiakili.

Taarifa kuhusu huduma za urgent care katika NSW

Idara za dharura katika NSW zina shughuli nyingi sana, na watu wengi wanakuja na mahitaji ya urgent care ambayo yangeweza kutibiwa haraka na vizuri na huduma nyingine za afya.

Serikali ya NSW imejitolea ufadhili wa dola milioni 124 kwa muda wa miaka miwili ili kutoa huduma 25 za urgent care katika NSW hadi kati ya mwaka ya 2025.

Upanuzi huu wa huduma za urgent care katika jumuiya za NSW husaidia idara za dharura kuzingatia wagonjwa mahututi au waliojeruhiwa.

Maswali yanayoulizwa mara nyingi kuhusu huduma za urgent care katika NSW

  • Urgent care ni uangalifu wa kimatibabu unaohitajika katika saa 2 hadi 12 kwa ugonjwa au jeraha ambalo halihatarishi maisha. Uangalifu huu wa kimatibabu unaweza kutolewa kwa usalama katika mpangilio wa huduma ya afya nje ya idara ya dharura.


  • Huduma ya urgent care ni huduma ya afya inayotoa utunzaji wa muda, na kwa mara moja kwa mahitaji ya afya yanayohitaji uangalifu haraka wa kimatibabu lakini hayahatarishi maisha.

    Huduma za urgent care hutolewa ana kwa ana au mtandaoni (kwa simu au kwa simu ya video).


  • Watu wanapaswa kutumia huduma ya urgent care kama wanahitaji matibabu ya haraka kwa suala la afya ambalo halihatarishi maisha, au kama hawawezi kupata miadi na daktari wa kawaida wa eneo (GP) kwa jambo la afya ambalo linapaswa kutibiwa.

    Huduma za urgent care zinawapa watu matibabu wanayohitaji haraka, bila kungoja kwenye idara ya dharura yenye shughuli nyingi.



  • Watu wenye umri wote wanaoishi katika au kutembelea NSW walio na mahitaji ya Urgent care wanaweza kupata huduma mbalimbali za urgent care za ana kwa ana na mtandaoni kwa kupiga simu kwa healthdirect kwa 1800 022 222. Kwa usaidizi wa lugha, watu wanapaswa kupigia simu kwanza kwa TIS Taifa kwa 131 450 na kuuliza  healthdirect.

    Healthdirect hupatikana kupigia simu bila malipo, saa 24 kwa siku, siku 7 kwa wiki. Wapigaji simu wanazungumza na muuguzi aliyesajiliwa ambaye anauiliza maswali kuhusu hali yao na kisha kuwaelekeza kwa utunzaji wanaohitaji katika mahali panapofaa kwa hali yao na eneo lao, ikiwa ni pamoja na lakini si tu kwa huduma ya urgent care.

    Kwa huduma fulani za urgent care za ana kwa ana, muuguzi wa healthdirect anaweza kuweka miadi kwa niaba ya mpigaji simu yule.

    Watu wanaopigia simu kwa healthdirect wanaweza kuomba kuzungumzia na muuguzi wa kiume au kike, wakipendelea.




  • Watu wenye matatizo ya kusikia au kusema wanapaswa kwanza kutembelea tovuti ya National Relay Service kwa About the National Relay Service​ ili kuchagua mbinu ya kutuma ujumbe kwa zamu unaofaa kwao na kuuliza  healthdirect.​




  • Watu wanapaswa kupiga simu ili kupata ambulensi kwenye Sifuri Mara Tata (000) au kwenda kwa idara ya dharura mara moja kama wana jeraha au ugonjwa mbaya au hali ya dharura yanayohatarisha maisha.

    Mifano ya dharura yenye kuhatarisha maisha inajumuisha:

    • kuanguka ghafla
    • shinikizo au maumivu ya kifua yanayodumu zaidi ya dakika 10
    • matatizo ya kupumua
    • kutokwa na damu isiyoweza kudhibitiwa
    • matatizo makubwa ya afya ya akili.

  • Ndiyo. Huduma za mkalimani hutolewa bila malipo kwa mtu yeyote anayeziomba au kuzihitaji.

    Watu hupata huduma za urgent care kwa kupigia simu kwa healthdirect. Kwa usaidizi wa wakilimani, watu wanapaswa kupigia simu kwanza kwa TIS Taifa kwa 131 450 na kuuliza healthdirect kwa 1800 022 222.

    Iwapo healthdirect ikiunganisha mpigaji simu pamoja na huduma urgent care ya mtandao kwa simu au video, mkalimani atahamishwa moja kwa moja na mpigaji simu, au healthdirect atapanga kwa mkalimani kuunganishwa kwa simu au simu ya video pamoja na mpigaji simu.

    Iwapo healthdirect ikiunganisha mpigaji simu pamoja na huduma urgent care ya ana kwa ana, huduma ile atashauriwa kwamba mkalimani anahitajika. Kisha itakuwa wajibu wa huduma ya urgent care kupanga upatikanaji wa muda mzuri kwa mkalimani, kwa ana kwa ana au kwa simu au video.



  • Kunapatikana anuwai ya huduma za urgent care za ana kwa ana na mtandao zinazotoa matibabu na ushauri kwa masuala ya afya ambayo yanahitaji uangalifu haraka wa kimatibabu.

    Baadhi ya huduma za urgent care za ana kwa ana zina vifaa na wafanyakazi wa kutibu magonjwa na majeraha mbalimbali ambayo sio hatari kwa maisha. Huduma kadhaa za urgent care za ana kwa ana hutoa pia huduma za eksirei na za magonjwa kwa wenye kadi za Medicare na wanaotafuta hifadhi katika jamii. Inamaanisha watu wanaweza kupata magonjwa au majeraha yao kusimamiwa haraka katika mahali pa moja.

    Huduma za urgent care za mtandao huunganisha watu kwa mbali kwa simu au video pamoja na wataalam wa afya ambao wanaweza kutiba na kushauri kuhusu mahitaji ya urgent care. Hawa ni pamoja na madaktari bingwa na wauguzi, wanaoweza kutathmini hali yao na kuwasaidia kupata matibabu na ushauri ufaao.


  • Ni ya bure kwa mtu yeyote kupigia simu healthdirect kwa 1800 022 222 na kupokea taarifa, ushauri au kuunganishwa na huduma ya kutunza afya, ikiwa ni pamoja na huduma ya urgent care.

    Matibabu yanayopitia huduma ya urgent care ni ya bure kwa watu walio na kadi ya Medicare na kwa watafutaji hifadhi wa jamii.




  • Huduma za urgent care zipo wazi kwa kawaida kuanzia saa 2 asubuhi hadi saa 2 usiku (8am hadi 8pm) kila siku ya wiki, pamoja na likizo za umma. Huduma kadhaa za urgent care za mtandao hupatikana, saa 24 kwa siku, siku 7 kwa wiki.

    Ili kupata huduma ya urgent care kwa kupigia simu kwa healthdirect kwa 1800 022 222, watu wanaweza kuunganishwa na huduma yenye kufaa na inayopatikana kwa mwelekeo wao.

    Healthdirect hupatikana kupigia simu bila malipo, saa 24 kwa siku, siku 7 kwa wiki kwa 1800 022 222.


  • Serikali ya NSW inafadhili utoaji wa huduma 25 za urgent care kote NSW, ambazo zote zitaanza kufanya kazi kufikia katikati ya mwaka ya 2025. Utoaji wa huduma hizi utaenea katika maeneo mbalimbali ya miji mikuu, mikoa na vijijini.

    Zaidi ya huduma hizi za ana kwa ana, huduma mbili za urgent care za mtandao zinapanuliwa kote jimboni:

    • Huduma ya urgent care ya mtandao ya GP - hutoa ufikiaji wa mbali kwa madaktari wa jumla (GPs).
    • Huduma ya virtualKIDS urgent care – huwapa watoto na familia zao ufikiaji wa mbali kwa madaktari wa watoto na wauguzi maalum wa watoto.

    Serikali ya Australia pia imejitolea ufadhili ili kutoa huduma za kiafya zinazotoa urgent care katika NSW, kupitia Medicare Urgent Care Clinics ambazo zinaanzishwa katika maeneo kadhaa ya NSW.


  • Healthdirect ni huduma inayofadhiliwa na serikali ambayo hutoa taarifa za afya na ushauri kupitia tovuti, app na simu ya usaidizi.

    Healthdirect husaidia watu kudhibiti afya yao wenyewe na kuwaunganisha na huduma sahihi katika mahali sahihi, ikijumuisha lakini bila kuweka mpaka kwa huduma ya urgent care.

    Simu ya msaada ya healthdirect hupatikana bila malipo, saa 24 kwa siku, siku 7 kwa wiki kwa 1800 022 222.

    Wapigaji simu wanazungumza na muuguzi aliyesajiliwa ambaye anauliza maswali fulani kuhusu hali yao na kisha kuwaelekeza kwenye huduma wanayohitaji katika mahali panapofaa kwa hali na eneo lao, ikijumuisha:

    • kutoa ushauri wa kutumia huduma inayofaa ya afya, inayopatikana katika eneo, pamoja na daktari wa kawaida (GP)
    • kuweka miadi katika huduma ya urgent care ya mtaa
    • kuunganisha mpigaji simu na mtaalam kama vile daktari wa kawaida (GP) au muuguzi wa watoto kwa simu au simu ya video
    • kutoa ushauri na usaidizi wa kusimamia suala la afya nyumbani
    • kupigia simu ambulensi au kumwelekeza mgonjwa kwa idara ya dharura ya karibu zaidi wakati unapofaa.


  • Kwa watu walio karibu na mpaka wa NSW

    Watu kadhaa wanaokaa au kutembelea majimbo na wilaya za Australia za nje ya NSW wanaweza kupata huduma za urgent care zilizopo NSW. Wapiga simu kwa healthdirect kwa 1800 022 222 wanaohitaji matibabu ya haraka , kama vile wale wanaokaa karibu na mpaka wa NSW, huenda kuunganishwa na huduma zilizopo katika NSW, ikiwa inafaa.

    Kwa watu katika majimbo na wilaya zingine za Australia

    Watu katika majimbo na wilaya zote za Australia isipokuwa Queensland wanaweza kupigia simu kwa healthdirect (inayojulikana kuwa NURSE-ON-CALL jimboni Victoria) kwa 1800 022 222 na kuunganishwa na huduma zinazofaa za afya zinazopatikana kwa eneo la mtaa.

    Watu wanaoishi au kutembelea Queensland wanaweza kupiga simu kwa 13 HEALTH (13 43 25 84) ili kuzungumzia na muuguzi aliyesajiliwa saa 24 kwa siku, siku 7 kwa wiki na kuunganishwa na huduma zinazofaa za afya zinazopatikana kwa eneo la mtaa.

    Medicare Urgent Care Clinics zinapatikana pia katika majimbo na wilaya zote za Australia.



  • Ndiyo. Kuna huduma mbalimbali tofauti za urgent care katika NSW. Nyingi zinapatikana kwa watu wa umri wote.

    Huduma kadhaa zinaundwa ili kutoa huduma mahususi kwa wazee.

    Huduma ya virtualKIDS urgent care imeundwa mahususi ili kutoa urgent care kwa watoto wenye umri hadi miaka 15.

    Kwa kupata huduma za urgent care kupitia healthdirect, watu wanaunganishwa na huduma ya kufaa kabisa kwa hali yao, eneo lao na umri wao.



  • Ndiyo. Watu wa umri wowote wanaweza kupigia simu kwa healthdirect.

    Mtoto mwenye umri wa miaka 16 au chini yake anapopigia simu healthdirect, muuguzi kwa kawaida atauliza kama kuna mtu mzima pamoja naye ambaye muuguzi anaweza kuzungumza naye. Ikiwa hakuna mtu mzima aliyepo, au mtoto anaomba faragha, muuguzi atamwuliza mtoto mfululizo wa maswali kuhusu hali yake ili kuamua huduma ya afya inayofaa zaidi kwa hali na eneo lake. Kisha muuguzi hutoa maelezo na ushauri wa kiafya unaolingana na umri wake au anamuunganisha mtoto na huduma ya afya inayofaa zaidi inayopatikana kwake.

    ​​

  • NSW Health inachukua ulinzi wa faragha ya afya na taarifa za kibinafsi kwa uzito na inalazimika kwa sheria kuheshimu na kudumisha haki za faragha za wagonjwa, wafanyakazi na wahusika wengine.

    Taarifa za kina kuhusu sheria na sera za faragha zinazotumika kwa NSW Health, na huduma za afya zinazotolewa na NSW Health, huweza kupatikana kwa tovuti ya NSW Health.


  • Kwa kupatikana huduma ya urgent care badala ya idara ya dharura kwa masuala ya afya ambayo si hatari kwa maisha, watu hupata matibabu wanayohitaji na kuepuka kungoja katika idara ya dharura yenye shughuli nyingi. Hii inapunguza shinikizo kutoka kwa idara za dharura, na kuziruhusu kuzingatia wagonjwa mahututi au waliojeruhiwa sana.

    Huduma kadhaa za urgent care za ana kwa ana hutoa huduma za eksrei na za magonjwa kwa wenye kadi za Medicare na wanaotafuta hifadhi katika jamii. Hii ina maana  kwamba watu wanaohitaji huduma hizi wanaweza kudhibitiwa kwa  haraka ugonjwa au majeraha yao katika sehemu moja.


  • Wagonjwa wanaotunzwa na huduma ya urgent care wanapaswa kuwashauri wafanyakazi mara moja ikiwa wanahisi kuwa wanazidi kuwa wagonjwa, au hali yao inazidi kuwa mbaya.

    Iwapo mgonjwa anazidi kuwa mgonjwa wakati anapotumia huduma ya urgent care, wafanyakazi wa kimatibabu na wauguzi watatathmini hali yake haraka na kuamua mahali pazuri zaidi kwa mahitaji yake ya utunzaji, pamoja na kupanga usafiri hadi idara ya dharura ikiwa hali yake imekuwa hatari kwa maisha.

    Wagonjwa na walezi wao wanaweza pia kupigia simu kwa Sifuri Mata Tatu (000) wakati wowote.


  • Tunakaribisha maoni yote, kwani hutusaidia kuelewa tunachofanya vizuri na jinsi tunavyoweza kuboresha huduma zetu za afya.

    Watu wanaopokea huduma kutoka healthdirect au kutoka kwa huduma ya urgent care wanaweza kuwasiliana kwa barua pepe au ujumbe wa maandishi ili kutoa maoni kuhusu matumizi yao.

    Watu wanaotaka kutoa maoni moja kwa moja kwa NSW Health au kwa healthdirect wanaweza kufuata mwongozo wa hapa chini:

    Ili kutoa maoni (pongezi, madokezo au malalamiko) kuhusu utunzaji unaopokelewa kupitia huduma ya urgent care, unaweza kutuambia kuhusu uzoefu wako kupitia tovuti ya maoni ya NSW Health.

    Ili kutoa maoni (pongezi, madokezo au malalamiko) kuhusu huduma ya healthdirect tafadhali tembelee tovuti hii.  



  • Taarifa zote na nyenzo za lugha kuhusu huduma za urgent care zinazotolewa katika NSW zinapatikana kwenye tovuti ya NSW Health.

    Taarifa na nyenzo zaidi kuhusu huduma za urgent care zinazotolewa katika NSW hupatikana katika Kiingereza kwenye tovuti ya NSW Health.


Current as at: Wednesday 13 December 2023
Contact page owner: System Purchasing