Je, kifua kikuu (TB) ni nini?

TB ni maambukizo yanayosababishwa na bakteria au vijidudu vya TB

TB inaenea kupitia hewani

TB huponywa kwa kutumia viuasumu maalum

Dalili za TB zinaweza kujumuisha

Kukohoa kwa muda zaidi ya wiki 2

Kikohozi chenye kamasi au damu

Homa, kuhisi baridi au jasho usiku

Kupoteza uzito haraka

Kujisikia uchovu kila mara

Kupoteza hamu ya kula

Uvimbe au maumivu

TB iliyofichwa au 'inayolala'

Vijidudu vya TB vinaweza kulala kwenye mwili wako na

Huwezi kueneza vijidudu vya TB kwa watu wengine

TB inayolala inaweza kuamka na kufanya uwe mgonjwa

Kipimo cha ngozi au kipimo cha damu cha TB kinaweza kugundua TB inayolala

TB inayolala inaweza kutibiwa na viuasumu maalum ili kuzuia vijidudu vya TB kuamka

Je, nani anaweza kuwa mgonjwa?

Watu ambao wameishi au walitumia muda na mtu mwenye TB

Watu wenye hali ya kimatibabu au wanapata tiba inayoathirika mfumo wao wa kinga

Watoto wadogo

Watu ambao walizaliwa au wameishi katika nchi zenye TB nyingi

Je, ninapaswa kufanya nini?

Mwone daktari (GP) wako au kliniki ya TB clinic ya eneo lako

Pata eksrei ya kifua

Toa sampuli ya mate

Upimaji na matibabu ya TB bila malipo

upimaji na matibabu ya TB ni bure kwa kila mtu kwenye kliniki za TB za NSW.

Kupata maelezo zaidi tembelea health.nsw.gov.au​.​

Current as at: Tuesday 9 June 2026
Contact page owner: Communicable Diseases